Skip to main content

JINSI YA KUJENGA NDOA BORA

NDOA ni shule pekee ambayo unapata cheti kabla ya kuanza masomo. Ni shule ambayo kamwe hauwezi kuhitimu.

Ni shule ambayo unatakiwa kuhudhuria siku zote za uhai wako. Ni shule ambayo hakuna likizo ya kuumwa au sikukuu.

Ni shule ambayo iligunduliwa na Mungu katika misingi ifuatayo;

1. Msingi wa upendo.

2. Kuta za shule zimejengwa kwa "uaminifu"

3. Madirisha yametengenezwa kwa "uvumilivu"

4. Samani zimetengenezwa kwa "msamaha"

5. Na ikaizekwa kwa "Imani"

Ukumbuke kuwa wewe ni mwanafunzi tu na sio mkuu wa shule ya NDOA. Mungu ndio Mkuu wa Shule.

Hata wakati wa mapito, majaribu, kimbunga na misukosuko ya hapa na pale usikimbie nje ya shule.

Kamwe usiende kulala kabla hujamaliza homework yako. Kamwe usisahau kusoma somo la mawasiliano. Wasiliana na mwanafunzi mwenzio pamoja na Mwalimu mkuu.

Kama utaona kuna kitu kwa mwanafunzi mwenzako ambacho kimsingi haukipendi, basi ukumbuke mwenzako nae ni mwanafunzi na sio mhitimu mwalimu Mkuu bado hajamalizana nae. Hivyo ichukulie ni changamoto na muifanyie kazi kwa pamoja.

Msisahau kusoma kitabu kitakatifu kilicho kwenye mtaala wa shule ya Ndoa (Biblia). Najua kuna muda unaweza ukajisikia kutokuhudhuria darasani lakini unatakiwa uhudhurie tu.

Utakapojaribiwa kuacha shule jipe ujasiri wa kuendelea na shule. Najua mitihani mingine ya muhula au nusu muhula inaweza kuwa migumu isiyo na majibu kwako.

Lakini kumbuka Mwalimu Mkuu anayo majibu tayari na anafahamu unaweza ukakabiliana nayo na anaona hiyo ndio shule nzuri kwako kuzidi nyingine.

Ni moja ya shule nzuri kabisa katika ulimwengu huu. Furaha, amani, na upendo husindikiza masomo ya kila siku.

Masomo mbalimbali hutolewa katika shule hii, ila somo kuu kuliko yote ni UPENDO.

Baada ya miaka yote ya kusoma kwa nadharia, ukijiunga na shule hii utasoma kwa vitendo.

Kupendwa ni kitu kizuri, lakini kupenda ni upendeleo wa vyote. Ndoa ni sehemu ya furaha. Inatakiwa kufurahia tofauti zenu na sio tofauti zenu ziwe chanzo cha kutoelewana.

Mimi nawatakia kila la kheri wote mliopo kwenye hii shule takatifu. Na wale ambao bado tumuombe mwenyezi Mungu ambae ni Mkuu wa Shule atuchagulie wanafunzi wenzetu walio bora ambao tutaweza kujiunga nao katika hii shule nzuri hapa Duniani.

Comments

Popular posts from this blog

AINA MBALIMBALI ZA JUICE ZA MATUNDA, NA FAIDA ZAKE KAMA DAWA MWILINI

Matunda ya asili ni tiba asilia. Pia mchanganyiko wa matunda haya asilia huweza kutengeneza juice tamu ambayo pia huweza kuwa tiba asilia. Zifuatazo ni baadhi ya Juice ambazo unaweza tengeneza wewe mwenyewe hapo nyumbani na zikawa ni kama tiba kwako; TUFAHA NA TANGO LA KAWAIDA Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa harufu mbaya mdomoni na hupunguza joto la mwili. CHUNGWA, TANGAWIZI NA TANGO Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa laini. Pia hupunguza joto la mwili. Kwa wale wenye matatizo ya kuwa na ngozi kavu, juisi hii itawasaidia sana. NANASI, APPLE NA TIKITIMAJI Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya kazi ya kuondoa chumvi nyingi mwilini, husafisha kibofu cha mkojo na figo. Juisi hii ni nzuri kwa wale wenye matatizo ya kibofu na figo au wanaotaka kujikinga na magonjwa hayo. APPLE, TANGO NA ‘KIWI’ Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi. Kiwi ni ...

JUICE BORA ZA MATUNDA NA FAIDA ZAKE KATIKA KUBORESHA AFYA YA MWILI

Juisi ni kinywaji bora na maarufu duniani, lakini ni vyeme ukajua juisi ipi ina faida mwilini na ipi haina faida yoyote. Katika zama tulizonazo, kumezuka aina nyingi za vinywaji vinavyoitwa juisi, wakati si juisi bali ni vinywaji vyenye ladha ya matunda mbalimbali. Juisi ni kinywaji kilichotengenezwa kutokana na tunda halisi au mboga na si mchanganyiko wa maji na kemikali nyingine zenye ladha ya matunda na kupewa majina kama juisi ya machungwa, nanasi, zabibu, n.k. Mara nyingi vinywaji hivyo huwekewa sukari na kemikali nyingine za kuhifahdia (preservertives) ili zisiharibike, ambavyo kiafya havikubaliki. Licha ya kutumia jusi halisi kama kinywaji tu, juisi pia hutoa kinga na tiba kwa maradhi mbalimbali. Iwapo mtu atatengeneza mchanganyiko maalum wa matunda na kutayarisha juisi maalum na kuinywa, anaweza kupata kinga na tiba ya matatizo mbalimbali ya kiafya kama ilivyoanishwa hapa chini: KAROTI+ KITUNGUU SWAUMU + EPO Juisi ya mch...

AINA ZA MATUNDA YENYE KUIMARISHA NA KUONGEZA MVUTO WA NGOZI YA MWILI

  APPLE: Hili ni tunda maarufu sana duniani lihusishwalo na wapendanao, lakini tunda hili pamoja na kupewa umaarufu mkubwa duniani na kuwa na vitamini na madini kibao, pia lina kazi kubwa sana katika kukupa muonekano mzuri wa ngozi ya mwili wako.Tunda hili husaidia kuboresha mzunguko wa damu mwilini pamoja na kuhifadhi ngozi isipoteze uhalisia wake.   PAPAI: Ni tunda sahihi kabisa katika kukupa ngozi yenye mafuta, kurudishia au kuziba sehemu zilizoumia na kunyofoka katika ngozi yako. Papai pia hunga'arisha rangi ya ngozi yako, yote haya hufanyika na enzyme inayotokana papai ambayo huitwa papain. Endapo kama unataka kutumia papai katika ngozi yako ya uso, basi chukua asali changanya na papai lililo iva na paka usoni kwako kwa dakika 10 kisha safisha, kisha utaona kitakachotokea katika uso wako, utaonekana kama ngozi ya mtoto wa siku mbili.   AVOCADO: Tunda hili limekuwa maarufu sana kwa kutengenezewa juice, lakini huenda watu wakawa ha...