Wanaume wenye viuno vikubwa wako hatarini kupata saratani ya tezi dume ,utafiti umebaini.
Utafiti huo ulifanywa kwa watu 140,000 kutoka mataifa nane ya Ulaya na kubaini kuwa viuno vikubwa huongeza uwezekano wa mtu kupata saratani hiyo kwa asilimia 13.
Utafiti huo uliowasilishwa katika mkutano wa ugonjwa wa kunenepa uliofanyika mjini Gothenburg nchini Sweden uliangazia ushirikiano wa vipimo vya mwili miongoni mwa wanaume walio katika umri wa miaka 50 na hatari za saratani ya tewzi dume katika kipindi cha miaka 14.(BBC)
Matunda ya asili ni tiba asilia. Pia mchanganyiko wa matunda haya asilia huweza kutengeneza juice tamu ambayo pia huweza kuwa tiba asilia. Zifuatazo ni baadhi ya Juice ambazo unaweza tengeneza wewe mwenyewe hapo nyumbani na zikawa ni kama tiba kwako; TUFAHA NA TANGO LA KAWAIDA Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa harufu mbaya mdomoni na hupunguza joto la mwili. CHUNGWA, TANGAWIZI NA TANGO Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa laini. Pia hupunguza joto la mwili. Kwa wale wenye matatizo ya kuwa na ngozi kavu, juisi hii itawasaidia sana. NANASI, APPLE NA TIKITIMAJI Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya kazi ya kuondoa chumvi nyingi mwilini, husafisha kibofu cha mkojo na figo. Juisi hii ni nzuri kwa wale wenye matatizo ya kibofu na figo au wanaotaka kujikinga na magonjwa hayo. APPLE, TANGO NA ‘KIWI’ Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi. Kiwi ni ...
Comments
Post a Comment