WAPENDAO NA WAPENDE Aah!! Moyo nchi ya kiza,, wewe pofu waendaje?? Mji hisia fukiza,, mwenzangu umechotaje?? mimi zimenitatiza,, machozi yanitokaje?? MIMI NALIVUA PENDO,, WAPENDAO NA WAPENDE Aah!! Nanena haya kwa ndani,, uwongo nitasemaje?? Utamu huo kinywani,, mapenzi umekaaje?? Niloipata tufani,, mapenzi yameumbwaje?? MIMI NALIVUA PENDO,, WAPENDAO NA WAPENDE Dah!! moyo unanisimanga,, maumivu yakataje?? Haya hayana nyakanga,, mwalimu kaumiaje?? Shetani nyumba kapanga,, wazimu kaingiaje?? MIMI NALIVUA PENDO,, WAPENDAO NA WAPENDE Doh!! sisemi naweka shonde,, waja mpate bwabwaje nafsi yangu ni kibonde,, utamu ningepataje?? Mbio nakwepa makonde,, na nyie mlitakaje?? MIMI NALIVUA PENDO,, WAPENDAO NA WAPENDE Dah!! Raha ya kuendeleza,, mwendo umepunguaje japo nisema naweza,, mawazo nikapambaje kumbe huitaji pweza,, mchuzi nitaunywaje MIMI NALIVUA PENDO,, WAPENDAO NA WAPENDE Duh!! Kukuru moyo kakara,, vuta vuta ngekujaje?? Mwili utake mitara,, nafsi nimechafukwaje?? Pen...